Nilitaka kusahau, kuzungumzia hili
Waliniomba wadau, Kina ticha STAMBULI
Nitasema angalau, namimi bila kujali
Nitaeleza kidogo, changamoto Mkalamo
Ngumu njia za riziki, asikudanganye mtu
Piga boda piki piki, ama kakate misitu
Ndo wengi wamediriki, kuhama miji ya watu
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Si swala la masihara, tunasema liko wazi
Hakuna hapa ajira, wala fursa za kazi
Vijana tunazurura ,wengine wezi wa NAZI
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Boda boda majiani, wanaipata shughuli
Mara “iweke pembeni”, mbona mebeba wawili
Sikwambii msituni, mejaa maliasili
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Kitegemea kilimo, mvua shida kwakweli
Zinaishia ngurumo, na kunyesha huko mbali
Mwaka ukipata chumo, njaa yaja kwenye vuli
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Ya zamani bado yapo, kwa visiki vya mpingo
Yanayoathiri pipo, kushushiana viwango
Yale ya papo kwa hapo, warogaji na mazongo
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Vijana wanojituma, kutwa kupigwa hasadi
Wanawarudisha nyuma, makusudi makusudi
Wakikwona umekwama, raho zao zafaidi
Hizi ndizo changamoto, hapa kijijini kwetu
Wako wanosema sema, ukipita unaisha
Ukikonda una ngoma, ndio imekukondesha
Wakiona umehama, umekimbia maisha
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Ishu Maadili mema, ni wachache siku hizi
Wamesema wamesema, bado hawasikilizi
Watoto watu wazima, ushenzi kisha ushenzi
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Watoto shule kwa fimbo, wanaongoza kufeli
Huiga mambo ya ng'ambo, ya viduku na singeli
Ukimuuliza kimombo, iz iz ni muhali
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Yanatosha nilosema, yaliyobaki navunga
Mule nilo kwama kwama, jua SIJUI KUTUNGA
Vina na sauti njema, nawaachia wahenga
Mimi bado ni mchanga, ndo mana sina fasihi
JAMANI NDUGU ZANGU MIMI BADO MUANDISHI MCHANGA SANA
Naomba usiache kukosoa pale ambapo unaona kuna makosa.
Asante sana.
Waliniomba wadau, Kina ticha STAMBULI
Nitasema angalau, namimi bila kujali
Nitaeleza kidogo, changamoto Mkalamo
Ngumu njia za riziki, asikudanganye mtu
Piga boda piki piki, ama kakate misitu
Ndo wengi wamediriki, kuhama miji ya watu
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Si swala la masihara, tunasema liko wazi
Hakuna hapa ajira, wala fursa za kazi
Vijana tunazurura ,wengine wezi wa NAZI
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Boda boda majiani, wanaipata shughuli
Mara “iweke pembeni”, mbona mebeba wawili
Sikwambii msituni, mejaa maliasili
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Kitegemea kilimo, mvua shida kwakweli
Zinaishia ngurumo, na kunyesha huko mbali
Mwaka ukipata chumo, njaa yaja kwenye vuli
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Ya zamani bado yapo, kwa visiki vya mpingo
Yanayoathiri pipo, kushushiana viwango
Yale ya papo kwa hapo, warogaji na mazongo
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Vijana wanojituma, kutwa kupigwa hasadi
Wanawarudisha nyuma, makusudi makusudi
Wakikwona umekwama, raho zao zafaidi
Hizi ndizo changamoto, hapa kijijini kwetu
Wako wanosema sema, ukipita unaisha
Ukikonda una ngoma, ndio imekukondesha
Wakiona umehama, umekimbia maisha
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Ishu Maadili mema, ni wachache siku hizi
Wamesema wamesema, bado hawasikilizi
Watoto watu wazima, ushenzi kisha ushenzi
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Watoto shule kwa fimbo, wanaongoza kufeli
Huiga mambo ya ng'ambo, ya viduku na singeli
Ukimuuliza kimombo, iz iz ni muhali
Hizi ndizo changamtoto, hapa kijijini kwetu
Yanatosha nilosema, yaliyobaki navunga
Mule nilo kwama kwama, jua SIJUI KUTUNGA
Vina na sauti njema, nawaachia wahenga
Mimi bado ni mchanga, ndo mana sina fasihi
JAMANI NDUGU ZANGU MIMI BADO MUANDISHI MCHANGA SANA
Naomba usiache kukosoa pale ambapo unaona kuna makosa.
Asante sana.

COMMENTS