yajue majina 25 ya Mitume.

Majina Ya Mitume 25 katika Quran Pamoja na kwamba inasemwa kuwa idadi ya Mitume wanafika hadi 124,000 kutokana na baadhi ya mapokez...

Majina Ya Mitume 25 katika Quran


Pamoja na kwamba inasemwa kuwa idadi ya Mitume wanafika hadi 124,000 kutokana na baadhi ya mapokezi, lakini Hadiyth hizo zimedhoofishwa na hivyo hatuwezi kuzitegemea, ila kuna Hadiyth ambayo Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) iliyosimuliwa na Abu Dhar ambayo alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) idadi ya Mitume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na akamjibu kuwa ni mia tatu na makumi kadhaa. Hadiyth hiyo imeelezwa usahihi wake na Imaam Al-Albaaniy kama ilivyo hapa chini:
  عن أبي ذر ، قال : قلت : يا رسول الله ! أي الأنبياء كان أول ؟ ! قال : آدم ، قلت : يا رسول الله ! ونبي كان ؟ ! قال : نعم نبي مكلم ، قلت : يا رسول الله : كم المرسلون ؟ ! قال : ثلاث مئة وبضعة عشر ؛ جما غفيرا . 
الراويأبو ذر الغفاري  -  خلاصة الدرجةصحيح  -  المحدثالألباني  -  المصدرمشكاة المصابيح  - الصفحة أو الرقم: 5669
Kutoka kwa Abu Dhar ambaye amesema: Nilisema: Ewe Mjumbe wa Allaah, Nabii yupi wa mwanzo? Akasema: ((Aadam)). Nikasema: Ewe Mjumbe wa Allaah, alikuwa ni Nabii? Akasema: ((Ndio Mtume aliyesemeshwa)) Nikasema: Ewe Mjumbe wa Allaah. Wapo Mitume wangapi? Akasema: ((Mia tatu na makumi kidogo)) [Mishkaat Al-Maswaabiyh ikiwa na daraja ya Swahiyh]
Hata hivyo idadi iliyotajwa katika Qur-aan ni Mitume 25 pekee na dalili ni kauli ya (Subhaanahu wa Ta'ala):
((وَرُسُلاً قَدْ قَصَصْنَاهُمْ عَلَيْكَ مِن قَبْلُ وَرُسُلاً لَّمْ نَقْصُصْهُمْ عَلَيْك))
((Na Mitume tuliokwisha kukuhadithia kabla yake, na Mitume wengine hatukukuhadithia)) [An-Nisaa: 164] 
Watume 18 wametajwa kwa pamoja katika Aayah 4 zifuatazo zinazofuatana:
((وَتِلْكَ حُجَّتُنَا آتَيْنَاهَا إِبْرَاهِيمَ عَلَى قَوْمِهِ نَرْفَعُ دَرَجَاتٍ مَّن نَّشَاء إِنَّ رَبَّكَ حَكِيمٌ عَلِيمٌ)) (( وَوَهَبْنَا لَهُ إِسْحَقَ وَيَعْقُوبَ كُلاًّ هَدَيْنَا وَنُوحًا هَدَيْنَا مِن قَبْلُ وَمِن ذُرِّيَّتِهِ دَاوُودَ وَسُلَيْمَانَ وَأَيُّوبَ وَيُوسُفَ وَمُوسَى وَهَارُونَ وَكَذَلِكَ نَجْزِيالْمُحْسِنِينَ))   ((وَزَكَرِيَّا وَيَحْيَى وَعِيسَى وَإِلْيَاسَ كُلٌّ مِّنَ الصَّالِحِينَ)) ((وَإِسْمَاعِيلَ وَالْيَسَعَ وَيُونُسَ وَلُوطًا وَكُلاًّ فضَّلْنَا عَلَى الْعَالَمِينَ))  
((Na hizo ndizo hoja zetu tulizo mpa Ibraahiym kuhojiana na watu wake. Tunamnyanyua kwa vyeo tumtakaye. Hakika Mola Mlezi wako ni Mwenye hikima na Mwenye ujuzi)). 
((Na tukamtunukia (Ibraahiym) Is-haaq na Ya’aquub. Kila mmoja wao tulimwongoa. Na Nuuh tulimwongoa kabla. Na katika kizazi chake tulimwongoa Daawuud na Sulaymaan na Ayyuub na Yuusuf na Muusa na Haaruun. Na hivi ndivyo tunavyowalipa wafanyao wema))
((Na Zakariyya na Yahyaa na ‘Iysaa na Ilyaas. Wote walikuwa miongoni mwa watu wema)) 
((Na Ismaa’iyl, na Al-Yasaa, na Yuunus, na Luutw. Na wote tuliwafadhilisha juu ya walimwengu wote)) [al-An’aam:  83-86]
Manabii na Mitume waliotajwa katika Qur-aan kwa mpangio wa ujio nikama ifutavyo:
1.                  Aadam.
2.                  Idriys.
3.                  Nuuh.
4.                     Huud.
5.                        Swaalih.
6.                        Ibraahiym.
7.                           Luutw.
8.                           Ismaa'iyl bin Ibraahiym.
9.                           Is-haaq bin Ibraahiym.
10.                        Ya'quub bin Is-haaq bin Ibraahiym.
11.                        Yuusuf bin Ya'quub bin Is-haaq bin Ibraahiym.
12.                        Shu'ayb.
13.                         Ayyuub.
14.                         Dhul Kifl.
15.                         Muusa.
16.                         Haaruun nduguye Muusa.
17.                         Daawuud.
18.                         Sulaymaan bin Daawuud.
19.                         Ilyaas.
20.                         Alyasa'.
21.                         Yuunus.
22.                         Zakariyya.
23.                         Yahya bin Zakariyya.
24.                         'Iysaa bin Maryam.
25.                         Muhammad. (Swalla Allaahu 'alayhim wa sallam)
Na Allaah Anajua zaidi








COMMENTS

Follow - ili usipitwe

Kwa mawasiliano zaidi

Name

Afya,66,Blogging,18,Burudani,29,Dini,99,Maisha,38,Mashairi,52,Sitosahau,37,Teknolojia,7,Usichokijua,14,
ltr
item
mrbunduki: yajue majina 25 ya Mitume.
yajue majina 25 ya Mitume.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh6uRBbx7lbOq6kQAWN3s0yXgUVkpXZjMaubLBGH84MDVIDZBD5mwftD7cTUepG0vFq19C5PBeLK8CYeoVJVU5FjnFp3dcBYc8jB3jTnxoF-7oJnD5V93dyX2svAS1mJqi8l5xptIKpzIo/s400/luxury-royal-25-wedding-anniversary_1340-6709.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh6uRBbx7lbOq6kQAWN3s0yXgUVkpXZjMaubLBGH84MDVIDZBD5mwftD7cTUepG0vFq19C5PBeLK8CYeoVJVU5FjnFp3dcBYc8jB3jTnxoF-7oJnD5V93dyX2svAS1mJqi8l5xptIKpzIo/s72-c/luxury-royal-25-wedding-anniversary_1340-6709.jpg
mrbunduki
https://sayyidbunduki.blogspot.com/2018/06/yajue-majina-25-ya-mitume.html
https://sayyidbunduki.blogspot.com/
https://sayyidbunduki.blogspot.com/
https://sayyidbunduki.blogspot.com/2018/06/yajue-majina-25-ya-mitume.html
true
3501413861140022348
UTF-8
Loaded All Posts Hakuna chapisho lolote View All Read more Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All Recommended posts LABEL ARCHIVE Search/Tafuta ALL POSTS Bahati mbaya, Ulichotafuta hakipo Rudi nyumbani/Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content