MwenyeziMungu amesema katika Qur an tukufu kuwa "Oeni katika mnaowapenda (wanawake) wawili, watatu na wanne. Na ikiwa mnahofu uadilifu basi mmoja"
Hapa baadhi ya watu (hasa wanawake wenyewe) huwa wanajiuliza na kulaumu kwanini iwe hivi? Wakihisi kama wameonewa ama hawakutendewa haki. Lakini ukweli ni kwamba ni sahihi kabisa
- Hizi ni sababu chache za kufahamu kwanini MWENYEZIMUNGU ameruhusu kuoa mke zaidi ya mmoja.
TWENDE PAMOJA
Mwenyezimungu ndiye aliyemuumba mwanaume na mwanamke na anawafahamu vizuri. Kwahiyo anayajua madhaifu ya mwanaume na anayajua madhaifu ya mwanamke.
- Kwanza Allah amemuumba mwanadamu na akampa matamanio ya kimwili ambayo kuyamaliza ni mpaka mtu apate mwenza. kwa kuliona hilo ndipo akaweka NDOA. Hii ni ili watu waepuke kufanya zinaa. Kwani zinaa ina madhara mengi katika jamii na katika dini.
Wataalamu wanasema - idadi ya wanawake iliyopo ukilinganisha na wanaume ni zaidi ya mara nne, yaani kila mwanaume mmoja angalau awe na wanawake wanne. Sasa je kama kila mtu akiwa na mwanamke mmoja waliobaki wengine watakwenda wapi?
KWANINI ALLAH AMERUHUSU KUOAMPAKA WANAWAKE WANNE?
A. MAUMBILE
Maumbile ya mwanaume haiwezekani kuvumilia kukaa na mwanamke mmoja (automatically)
Yaani mwanamke anaweza kuvumilia kukaa muda mrefu bila kukutana na mwanaume kimwili... Kitu ambacho kwa mwanaume aliyetimia haiwezekani. Hivyo mwanamke mmoja akiwa mbali na mumewe basi mwingine atakuwepo kumliwaza bwana yule.
B. LIKIZO
Mwanamke ana likizo nyingi Sana katika maisha yake ya kila siku ambazo zitamfanya mwanaume asipate tendo la ndoa. Baadhi ya likizo hizo ni kama vile;-
KWANINI ALLAH AMERUHUSU KUOAMPAKA WANAWAKE WANNE?
A. MAUMBILE
Maumbile ya mwanaume haiwezekani kuvumilia kukaa na mwanamke mmoja (automatically)
Yaani mwanamke anaweza kuvumilia kukaa muda mrefu bila kukutana na mwanaume kimwili... Kitu ambacho kwa mwanaume aliyetimia haiwezekani. Hivyo mwanamke mmoja akiwa mbali na mumewe basi mwingine atakuwepo kumliwaza bwana yule.
B. LIKIZO
Mwanamke ana likizo nyingi Sana katika maisha yake ya kila siku ambazo zitamfanya mwanaume asipate tendo la ndoa. Baadhi ya likizo hizo ni kama vile;-
(i) Mimba (Hasa inapokomaa)
(ii) Baada ya kujifungua,
(iii) Mzu8nguko wa hedhi
C. UCHUMI
Tukiachana na suala la mihemko ya kimwili, lakini pia mwanamke ni dhaifu katika kujitafutia riziki. Na hakuumbwa kuja kutafuta ila ameumbwa kwa ajili ya mwanaume... Na mwanaume ndiye mtafutaji. Utandawazi tu ndio umemfanya mwanamke leo kutafuta haki sawa na mwanaume.
Ulimwengu na uzungu ndo vitu vinavomtia kiburi mwanamke na kujiona ni sawa na mwanaume. Lakini mwanamke atabaki kuwa mwanamke tu milele.
SABABU Hizi ni chache kati ya nyingi ambazo zinafanya mwanaume aoe mwanamke zaidi ya mmoja.
ZINGATIA (MUHIMU)
Hii ni ruksa na sio lazima kuoa mke zaidi ya mmoja kwa sababu unatakiwa uwe muadilifu. Na Kama utashindwa baki tu na mke mmoja.
MUNGU ANISAMEHE KWA PALE NILIPOTELEZA (YEYE NDIYE AJUWAE)
Ahsante.
Imeandaliwa na
MRBUNDUKI.COM
COMMENTS