Maisha kwa mwanadamu, ma’na yake ni kuishi,
Tangu siku ya Adamu, hadi ile ya mazishi,
Maisha hutugharimu, kupata kila utashi,
Maisha uhusiano, mwema katika jamii.
Tangu siku ya Adamu, hadi ile ya mazishi,
Maisha hutugharimu, kupata kila utashi,
Maisha uhusiano, mwema katika jamii.
Tuko katika maisha, yaliyo na kila tabu,
Tuko tunayaendesha, tofauti na mababu,
Yote tunayadumisha, kila mtu kwa wajibu,
Maisha uhusiano, mwema katika jamii.
Tuko kwenye hali ngumu, ya uchumi kimaisha,
Ni wachache wanadamu, nuru wamefanikisha,
Baadhi ubinadamu, nadra kutuonyesha,
Maisha uhusiano, mwema katika jamii.
Tuko tunayaendesha, tofauti na mababu,
Yote tunayadumisha, kila mtu kwa wajibu,
Maisha uhusiano, mwema katika jamii.
Tuko kwenye hali ngumu, ya uchumi kimaisha,
Ni wachache wanadamu, nuru wamefanikisha,
Baadhi ubinadamu, nadra kutuonyesha,
Maisha uhusiano, mwema katika jamii.
(Charles Mloka, Diwani ya Mloka.)

COMMENTS