TWENDE SHAMBANI - (RIWAYA)

  SURA YA KWANZA UKODISHAJI WA SHAMBA Baada ya kupata wazo la kulima, tulianza kuulizia mahala ambapo tunaweza kupata shamba kwa ajili y...

 

SURA YA KWANZA

UKODISHAJI WA SHAMBA

Baada ya kupata wazo la kulima, tulianza kuulizia mahala ambapo tunaweza kupata shamba kwa ajili ya kukodisha. Maeneo ambayo tunafanya kazi (UHINDINI – MBEYA) kulikuwa na jirani yetu ambae alikuwa anafanya kazi ya ulinzi katika Bank ya Equity, ambaye alijulikana kwa jina la Shega. Kwa kuwa huyu alikuwa ni mwenyeji wa huku tuliona ni bora kufanya mawasiliano nae afanye michakato.

 

Baada ya muda alitupa majibu kuwa alipata shamba maeneno fulani katika Wilaya ya Mbozi Mkoa huu wa Mbeya. Hivyo alizungumza na jamaa zake wa huko. Jambo lilipokuwa tayari tuliamua kwenda na kuliona hilo shamba na kufanya makubaliano. Tulipanga siku rasmi ya kwenda huko.

 

Siku ya jumapili tarehe 15/10/2017 ndio siku ambayo tuliamua kwenda huko shambani. tulianza safari majira ya saa 4 za asubuhi tukiwa watu wane ambao ni bwana Ummari (Baba la baba), Afande Shega, Ben Oiso pamoja na Mimi (Saidi Bunduki). Kiongozi wa safari hii alikuwa ni bwana Ummar (Baba la baba). Sehemnu ambayo tulikuwa tunakwenda ni kijiji kiitwacho Senjele. Kijiji ambacho kinapatikana takriban kilomita 45 kutoka Mbeya mjini kuelekea TUNDUMA.

 

Safari hii ilikuwa ni kwajili ya kwenda kuliona shamba ambalo tumekusudia kukodisha kwa ajili ya kilimo cha mahindi. Tulifika Senjele  majira ya saa 6 mchana na kumsubiri mwenyeji wetu ambaye ndiye aliyekuwa amefanya michakato ya kutafuta hilo shamba. Jamaa yule anaitwa SIMON alikuwa anatokea Songwe. Huyu ndiye alikuwa na mawasiliano na bwana Shega. Baada ya muda kidogo alikuja na kutukuta tumekaa chini ya muembe mdogo uliopo pale njiani kijijini.

Lakini pia kuja kwake bado haikuwa mafanikio kwa sababu, huyo bwana ambaye ndiye mwenye shamba alikuwa hayupo, hivo bado kulikuwa na haja ya kumsubiri na kufanyanaye maelewano kuhusu shamba. Pia muda ule tuliutumia kwa ajili ya kwenda kuliona hilo shamba ambalo lilikuwa linasemekana kuwa lilikuwa na ukubwa wa ekari sita. Kwa bahati nzuri shamba halikuwa mbali na bara bara kuu ya Tunduma.

 

Pia tulifurahi kuona shamba likiwa katika hali nzuri sana. Hii ni kwa sababu msimu uliopita lililimwa na baada ya hapo pia lilisafishwa kwa ajili ya kujiandaa na kilimo cha mwaka huu. Kwahiyo halikuwa na miti wala majani. Labda tu lilikuwa na haja ya kuchimbua tena na ng’ombe kwa ajili ya kuboresha zaidi. Na pia kwa kuwa tulikuwa tumechelewa kutafuta mashamba, haikuwa rahisi kwa muda ule kupata shamba kwa urahisi na hata kama tungepata isingekuwa rahisi kupata shamba lililo karibu na makazi ya watu au barabara kama vile.

 

Mpaka muda huu tulikuwa watu watano, kwa sababu tayari alikuwa ameshaongezeka jamaa mmoja (Simon). Huyu jamaa anaishi katika Kijiji kinachoitwa NANYALA. Nanyala ni kijiji kilicho nyuma kidogo ya kile kijiji cha Senjele. Hivi ni vijiji ambavyo vina mchanganyiko wa makabila ya Wanyakyusa na Wanyiha. Na haya miongoni mwa makabila makubwa Mkoani Mbeya.

Picha halisi ikionesha shamba jinsi lilivokuwa siku ya kwanza ambayo tulifika SENJELE.                              (Picha na Omy Krish)

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


Upande mwingine wa shamba. Kwa mbali zinaonekana nyumba za kijiji cha Senjele

 

 

Tulilikagua vema na kuridhika nalo kwa wakati huo tukimsubiri bwana NICKSON ambaye ndiye mwenye eneo lile. Lakini baada ya kufanya mawasiliano naye iligundulika kuwa alikuwa mbali kidogo na pale hivo aliomba kama kuna uwezekano tufanye maelewano na mke wake. Tulifanya hivyo lakini mwishowe mke wake alishindwa kufanya makubaliano kwa sababu alikuwa na hofu juu ya kupunguza bei. Kwa hiyo ilitulazimu kumsubiri bwana Nick.

Mpaka muda ule tayari ilikuwa ni saa nane za mchana na njaa zilianza kututafuna. Hivyo ilibidi tuangalie sehemu ya kupata chakula. Kwakweli sehemu ya kupata chakula kidogo ilikuwa ni changamoto kwa sababu Senjele ni kijijini sana hivyo hapakuwa na migahawa ya kutosha.              Lakini baadaye jamaa ambaye ndiye alikuwa mwenyeji wetu ambaye ni SIMON alitupeleka sehemu ya pili ya mji ule ambapo tulifanikiwakupata huduma ya chakula. Tulifanikiwa kupata wali maharage pamoja na nyama za kuchoma za mbuzi.

 

 

 

 

 

Sehemu ya kupata chakula. Hapa ni Saidi Bunduki akiwa na Ben Oiso. Hii ni sehemu ya nje ya Mgahawa. (Picha na Omy Krish)

Ndani ya Mgahawa, ulaji wa nyama ukiendelea. Pichani ni Baba la baba akitoa maelezo kwa ufupi kwa waaandishi juu ya safari yao kwa ujumla. (Picha na bunduki.com)

 

Baada kupata chakula, watu wakirudi shambani kuelekea na majukumu mengine – Kutoka kushoto ni Ben Oiso, Saidi Bunduki, Mr Shega na Simoni (Mwenye flana nyeupe)

Tulipomaliza kula chakula kile cha mchana tulirudi kule shambani na kumkuta bwana NICKSON ameshafika na alikuwa anatusubiri. Baada ya sisi kufika tulirudi tena shambani na tulielewana na kufika lengo. Kisha akaitwa Mwenyekiti wa Kijiji kwa ajili ya maandikishiano.

 

 

 

Picha iliyopigwa kutoka juu ikimuonesha Mwenyekiti.Huu ni Mkataba baada ya kukamilika

Akiwa katika harakati za kuandika Mkataba wa shamba

 

Shamba lilikuwa na ekari sita, na kila ekari moja tulikubaliana ni shilingi elfu 80. Lakini siku ile tulilipa pesa ya ekari moja tu na kuahidi kulipa kiasi kilichobaki siku nyingine. Baada ya pale muda ulikuwaumekwenda sana na tukaamua kurudi nyumbani. Tulifika nyumbani MBEYA MJINI mnamo majira ya saa moja usiku.

 

Safari ile ilikuwa tamu sana kwa kila aliyehudhuria pale kwani ilikuwa ni mfano wa safari ya watalii waliotembelea MLIMA KILIMANJARO huko Moshi. Kwani kila mtu miongoni mwenu alikuwa na furaha na bashasha sana. Wananchi wa kijiji kile walitushangaa sana kwani tulionekana kuwa moja kwa moja ni wageni tena wenye pesa zao.                                           Kumbe ha ha haaa.

KUMALIZIA MALIPO YA SHAMBA

Siku ya jumapili tarehe 05/11/2017. Safari hii tulikwenda mimi na Bwana Ummar kwa ajili ya kumalizia pesa iliyobaki katika malipo ya shamba. Tulikwenda  mara moja na kurudi. Safari hii tulikutana na yule bwana Simon ambaye yeye anakaa katika Kijiji cha Songwe. Kiasi kilichobaki kilikuwa ni shilingi laki nne (400,000/=). Tulipomaliza kuandikishiana kama kawaida tukaingia dukani na kunywa soda kisha tukasubiri gari na hatimae kurudi nyumbani mapema. Safari hii ya pili haikuwa na mambo mengi kama ile ya kwanza. Ilikuwa ni kwa ajili ya kukamilisha muamala wa pesa tu.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

SURA YA PILI

KUANZA KULIMA SHAMBA

 

Safari hii ilikuwa ni kwa ajili ya kwenda kufanya mipango ya kulima lile shamba.Safari hii ilikuwa ni siku ya jumapili tarehe 26/11/2017

Washiriki katika safari hii walikuwa ni MR UMMAR na MKE WAKE, BEN OISO, RAMADHANI CHIKUMBII, PAMOJA NA MIMI (Saidi Bunduki)

 

Tuliondoka Mjini Mbeya mnamo majira ya saa 5:44 asubuhi na kufika Mbalizi saa 6 mchana. Tulikaa Mbalizi takriban muda wa lisaa ili kusubiri gari iondoke. Ilipofika saa 6:57 mchana gari iliondoka na kufika SENJELE saa 6:40 mchana.

 

Safari hii ilikuwa ni kwa ajili ya kwenda kukamilisha suala zima la ulimaji. Pia kwa kuwa kulikuwa na vibarua walikwishaanza kulima hivo tulikwenda kutazama kazi walioifanya pamoja na kuwapelekea pesa yao. Tulipofika shambani walikuwa wamelima kama kiasi cha ekari moja kasoro hivi. Lakini siku ile hatukumkuta mwenyeji wetu ambaye ndiye alikuwa ametutafutia vibarua wale, na tulipofanya naye mawasiliano alikuwa kidogo ametoka na isingekuwa rahisi kufika kwa muda ule. Hivyo alitoa idhini kuwa pesa tuliokwenda nayo tumkabidhi mke wake kwani angeikuta tu, nasi tukafanya hivo.Ulipofika muda wa saa nane mchana kama kawaida tulielekea kule kule kwenye maeneo yetu ya kupata chakula cha mchana. Na mambo yalivyokuwa  siku hiyo utajionea hapo katika ukurasa ufuatao.

 

 

 

Baadhi ya vijana wakiwa na bashasha maeneo ya mgahawani wakisubiri chakula. Kutoka kushoto ni Ramadhani Chikumbii, Saidi Bunduki na Ben Oiso. (picha na Omy Krish)

 

Tulikaa kule shamba mpaka majira ya saa 10 jioni na kumaliza mambo ambayo yalitupeleka kule. Miongoni mwa mambo hayo ni kuweka mikakati mizuri ya kulima. Pia kwa uzuri zaidi wakulima walikuwa wameshaanza kazi yao. Hivyo katika pesa ambayo walikuwa wanaitaka (200,000/=) tuliwaachia advance ya shilingi laki moja na elfu ishirini.

Tuliondoka Senjele mishale ya saa 9:41 jioni na kufika Mbeya saa 10:50 jioni.

 

TANBIHI& MAELEZO YA ZIADA:-

Kama utafuatilia kwa makini utagundua kuwa kutoka Mjini mpaka shambani palikuwa na muda wa kama lisaa hivi. Na kwa upande wa nauli ilikuwa ni shilingi elfu mbili (2,000/=) kwa kila mtu mmoja. Kwahiyo utaona ni pesa kiasi gani ilikuwa inatumika katika usafiri. Pia tulilazimika zaidi kusafiri siku za jumapili kwa sababu ndio siku ambayo tunakuwa na nafasi kutokana na kazi yetu.

SURA YA TATU

UNUNUZIWA MBEGU NA UPANDAJI

Mnamo tarehe 02/12/2017 siku ya alhamisi. Alikuja bwana Simon kutoka Songwe. Hiii ni kwa ajili ya kushirikiana nasi katika suala la ununuzi wa mbegu. Alifika mnamo majira ya saa nane mchana. Baada ya muda aliondoka na bwana Ummar kuelekea sokoni kwa ajili ya kufanikisha suala hilo  na mambo yalikwenda kama yalivokusudiwa. Mbegu tulizokusudiwazilikuwa ni aina mbili ambazo ni PANNAR na SEEDCO. Simon alitangulia na ile mbegu kabisa ili iwe rahisi kwa wapandaji.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


Mr. Simon (kulia) akiwa katika duka la mbegu                 Aina ya mbegu ambazo zilinunuliwa

Maeneo ya sokoni (Mwanjelwa – Mbeya)

 

Ili kupunguza gharama tuliona ni bora kuenda kusaidia suala la upandaji katika moja ya siku. Na ilikuwa ni vema zaidi kuenda kupanda siku ya jumapili. Hivo tuliwaomba wale wapigaji mashimo waifanye kazi hiyo siku ya jumamosi. Lakini kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao haikuwezekana kufika katika siku hiyo. Na badala yake alifika mtu mmoja tu tena siku ya kuamkia jumatatu. Hivyo hatukuweza kwenda wote. Ila alikwenda kusimamia suala hilo bwana Simon kutoka Songwe.

Na baadaye bwana Ummar na Ben walikwenda kukamilisha baadhi ya malipo tu kwa vibarua. Hii ilikuwa ni tarehe 4/12/2017 siku ya jumatatu.

 

 

UOTAJI NA UKUAJI WA MAZAO

Tunamshukuru Mungu baada ya wiki mbili hivi mahindi yalikuwa tayari yameota na kunawiri vizuri. Ingawa kulikuwa na baadhi ya maeneo kidogo yalikuwa hayajaota vizuri lakini kwa asilimia kubwa shamba lote lilikuwa limeota vema.Siku ya jumapili ya tarehe 17.12.2017 tuliamua kutembelea shamba ili kuendelea na ukaguzi wetu kama kawaida. Kwakuwa siku hii ndio tunakuwa na nafasi ya kutosha kutokana na kazi zetu. Hivyo tulipata fursa ya kuelekea shamba Mimi na bwana Ummar. Kweli tulikuta hali ni nzuri kwa asilimia kubwa. Na mambo yalikuwa kama hivi;-

 

 

 

 


                                                

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Baba la baba akiwa katika ukaguzi shambani. (Picha na bunduki.com)

Picha ikimuonesha Bunduki akila embe chini ya muembe shambani baada ya kumaliza ukaguzi. (Picha na Omy Krish)

 

Kwakuwa  mahindi bado yalikuwa madogo na palizi ilikuwa bado haijashamiri. Hivyo baadhi ya wataalamu walishauri kuwa kwa muda ule tuache kwanza. Tusipige mbolea wala dawa ya kuuwa majani. Walishauri tusubiri kwa muda kama wa wiki mbili au tatu ili majani yaote na tupige dawa ya kuuwa majani.

 

Tulisuibiri kwa muda huo na siku moja katikati ya wiki tuliamua aende mmoja kwanza kukagua maendeleo ya shamba. Kwahiyo ilibidi Bwana Ummari na Ben Oiso waende maramoja na kukagua maendeleo ya shamba. Na hali waliyoikuta shamba ilikuwa kama utakavoona hapo chini katika picha. Kuna baadhi ya sehemu zilikuwa bora Zaidi, nyingine zilikuwa wastani wakati nyingine zilikuwa zimedhoofika zaidi.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


sehemu “A” ya shamba ikiwa na mahindi yenye afya bora.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


Sehemu “B” ya shamba ikiwa na mahindi yenye afya nzuriya wastani

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


sehemu “C” ya shamba ikionesha mahindi yakiwa na afya iliyodhoofika na wakati huo huo kukiwa na majani makubwa ambayo yalistahili kupaliliwa au kupigwa dawa.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

SURA YA NNE

PALIZI, MBOLEA NA DAWA YA KUKUZIA

Mpaka hapo sasa ulikuwa ni muda muafaka wa kufanya palizi. Na michakato ya kuwatafuta watu wa kupalilia ilianza rasmi. Lakini kwa bahati mbaya kila ambaye alipewa kazi ile alishindwa kutekeleza kutokana na sababu zake mwenyewe binafsi ambazo hazieleweki. Kutokana na sababu ya kukosekana kwa vibarua kwa muda muafaka hivyo mahindi yalianza kudhoofika taratibu hususan kwa sehemu “C” hii ambayo ilikuwa haikuota vizuri na pia tayari ilikuwa na majani makubwa.

 

Baadaye tuliamua kupiga dawa ya kuuwa majani tu ili angalau kuyanusuru mahindi haya. Siku moja tulimwambia bwana simon aje mjini huku Mbeya ili kusaidiana katika suala la utafutaji wa dawa ya kuuwa majani. Lakini pamoja na dawa pia tuliona ni bora kutafuta na mbolea kabisa ili wakati majani yanapigwa dawa ili yafe, huku nako mahindi yanapigwa mbolea ili yakue. Yaani tuliamua kufanya kazi mbili kwa wakati mmoja.

 

Bwana Simon aliamua kuacha kazi zake na kuja mjini kama kawaida na kushirikiana nasi katika suala la kutafuta dawa na mbolea. Kwakweli kijana huyu ni mfano wa kuigwa kwani alikuwa anajitolea sana katika hili bila kutaraji malipo yoyote.  Ni kwamba ni mtu mwenye msaada mkubwa sana katika kuhakikisha masuala yetu yanafanikiwa. Tulimshukuru sana kwa msaada wake.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


Picha zikiwaonyesha baadhi ya washiriki wa zoezi la kutia mbolea wakiwa katika harakati za kuchanganya mbolea ya UREA na DAP.                                                                                   (Picha ya kushoto ni SIMON, kulia ni SIMON na BUNDUKI)-Picha na Omy Krish

BABA la BABA (Upande wa kushoto) akiwa na BUNDUKI (kulia) wakiwa katika zoezi rasmi la utiaji wa mbolea – shimo hadi shimo.

 

 

Siku ya kwenda kusaidia kazi ya kuweka dawa na mbolea ilikuwa na maandalizi ya kutosha. Nyumbani tuliondoka watu watatu MIMI, UMMAR na MKE WAKE. Kwa kuwa kipindi hiki tulikuwa na gari ya ofisi hivyo haikuwa shida sana katika masuala ya usafiri na usafirishaji. Tukiwa na mifuko yetu miwili ya mbolea na vidumu viwili vya dawa tulianza safari asubuhi majira ya saa mbili. Tulipofika sehemu inayoitwa AYASI tuliwapitia bwana SIMON na kijana wake moja. Kwahiyo tukawa watu watano kwenye gari. Tulipofika shambani tukawapata na watu wenginne wawili, mmoja alikuja kwa ajili ya kupiga dawa na mwingine alisaidiana nasisi kuweka mbolea.

Huyu naye alikuwa pia anaitwa SIMON.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


Jamaa aliyekuwa anapiga dawa ya kuuwa majani (Jina limehifadhiwa)-picha na Omy krish

 

Katika upande wa mbolea tulichanganya mbolea za aina mbili ambazo ni DAP na UREA. Hii ni kutokana na maelekezo ya wataalam wetu. Kazi ya kuweka dawa na mbolea ilikuwa kubwa sana, hata ilipofika majira ya saa saba mchana watu walianza kuumwa na njaa ingawa mamayetu                                                    (MKE WA BWANA UMMAR) aliandaa chai na kwenda nayo kule shambani lakini mpaka muda ule njaa ziliuma na watu kuhitaji chakula cha mchana. Hivyo tulitoka na gari mimi na bwana Ummar na mkewake kwenda kutafuta chakula cha mchana.

 

Tulikwenda pale bondeni ambako huwa sikuzote ndipo tunapopata chakula cha mchana, lakini siku ile hapakuwa na huduma yoyote ya chakula. Kwahiyo ilitulazimu kuendelea mbele (SENJELE YA PILI) kuangalia kama tutapata mgahawa na kupata chakula. Lakini pia hapo Senjele ya pili hapakuwa na huduma yoyote ya chakula  kwani watu wengi walikuwa wapo Makanisani.

 

Tuliendelea tena mpaka mahala panapoitwa“Njia panda ya Iyula”  pia tukakosa chakula na kuendelea katika kijiji cha mbele yake kiitwacho RWANDA na hapondio tukabahatika kupata chakula. Tulipata wali na maharage. Tulikula na kuwabebea wenzetu ambao walikuwa wamebakia kule shambani. Baada ya kumaliza kula tunakuja kugundua kuwa kumbe pale hotelini huwa wanauzaga na kitimoto. Duhh simchezo, tulibaki kucheka na kuondoka.

 

Jua lilipozama watu walikuwa wamechoka sana. Lakini pia kazi iliyofanyika ilikuwa ni kubwa mno. Lakini pamoja na hayo pia kulikuwa na sehemu iliyobaki ambayo ilitakiwa kumaliziwa kesho yake. Hii ni kutokana na kuisha kwa muda, pia dawa ilikuwa imeisha.

Kwahiyo tulirudi nyumbani kwa makubaliano kuwa kesho yake wale jamaa waende wakamalizie na pia Ummar aende akasimamie na kuwalipa malipo yaliobakia. Jumatatu ilikuwa ni siku iliyofuata na bwana Ummar alikwenda na Ben Oiso ili kuhakikisha kuwa lile suala linakwenda kama lilivotakiwa. Na tunashukuru mambo yakaenda kama yalivopangwa. Ummar na Ben walishirikiana na vibarua wale kuhakikisha suala linakwenda vizuri. Tulimshukuru Mungu kwa kazi ile kuisha salama.

Mr Ben Oiso akiwa katika pozi. Hii ni ile siku ya pili alipokwenda na Mr Ummar (Baba la baba)- Picha na Omy Krish

 

Dawa ya kuuwa majani humwagiliwa kwa kutumia mitungi ya kumwagilia dawa kama ulivoona katika picha hapo juu. Na dawa hii inatakiwa baada ya kumwagiliwa kusiwe na mvua ndani ya siku ile ili iweze kufanya kazi barabara. Kwani mvua ikinyesha kabla ya dawa kuyakausha majani huweza kuiyayusha na kutokufanya kazi kama inavyopasa. Kwa bahati mbaya siku ile ile tu mvua ilianza kunyesha tukiwa kule kule shambani. Kwakweli ilikuwa mtihani, kwani majani hayakuweza kuungua kama tulivokusudia.

 

*************************

 

Siku moja bwana Ummar akiwa na BEN na ADAMU wa SMILE walikuwa wanatoka VWAWA kwa shughuli za kiofisi. Lakini wakati wa kurudi waliona ni vema kupitia shamba kuangalia maendeleo. Lakini kwa kweli mahindi bado hayakuwa katika hali nzuri kwahiyo bwana ADAM alishauri tununue dawa ya kuyapa nguvu mahindi na kukuwa kwa haraka (buster). Hivyo tuliona ni bora kufuata ushauri huu.

 

Jumapili iliyofuata ilikuwa ni tarehe,,,,,,,,,,,,,,tulifunga safari ya kuelekea shambani. Tukiwa MIMI, UMMAR na MKEWAKE, ADAM (smile) pamoja na BEN Oiso. Safari hii ilikuwa maalum kwa sababu ya kwenda kupiga mbolea ya kubust mahindi.Tulipofika shamba hatukuwakuta wenyeji wetu hivyo tulisumbuka kidogo kaitika suala la kupata dumu la kumwagilia pamoja na ndoo za maji. Lakini bwana Nick                                       (mwenyeji wetu/mwenye shamba) alisema kuwa dumu lake lilikuwa na hitilafu ya spring ya kumwagilia. Hivyo tutatufe spring hiyo ili tukifika tukachukue dumu hilo.

Lakini kutokana na kutofahamu kitu hicho, tulichukua kifaa ambacho hakikuwa sahihi na ikatulazimu baada ya kufika tukaazime dumu lingine.

Baada ya kufanikiwa kupata dumu tulikwenda nyumbani kwa bwana NICK na kuchukua ndoo na madumu na kushuka barabarani kuchukua maji. Tulipandisha maji shambani na hatimae watu kuanza kazi kama kawaida. Bunduki ndiye alianza kubeba mtungi kama utakavomuona hapo chini.

Wanaume wa kazi wakiwa katika zoezi la uchanganyaji wa mbolea (Booster)                                 Kuanzia kulia ni ADAM (smile) , BEN, UMMAR (aliyeshika kopo la maji safi) kishoto ni jamaa aliyetuazimia dumu la kumwagilia (Hakupenda jina lake litajwe)- picha na BUNDUKI

Bunduki akiwa katika kazi ya umwagiliaji wa dawa ya kukuzia (Picha na OMY KRISH)

BABA la BABA akiwa katika shughuli ya umwagiliaji wa dawa ya kukuzia.                                     (Picha na Bunduki.com)

 

Shughuli iliendelea kwa muda mrefu sana mpaka ilipofika majira ya saa saba mchana watu waliamua kula chakula. Kama kawayda mama yetu tuliyekwenda naye (MKE WA UMMAR) alitugawia chakula na kula. Baada ya kula watu waliendelea na kazi mpaka ilipofika majira ya saa kumi na moja jioni kila mtu alikuwa hoi bin taabani. Baada ya kumaliza kazi tuliweka alama mahala tulipoishia na kutafuta sehemu ili kupumzika na kujiandaa na kurudi nyumbani.

 

Uchovu baada ya kazi. Hapa ni mapumziko na stori kidogo baada ya kazi nzito                                             (Kutoka kulia ni Ummar, Adam na Bunduki) – picha na BEN OISO.

 

Baada ya hapo tulirudi nyumbani na kufika salama kuendelea na majukum mengine ya kujenga taifa. Pia tulitoa shukrani za dhati kwa bwana Adam kutoka kampuni ya SMILE COMMUNICATION kwa ushirikiano wake nasi katika kufanikisha zoezi hili. Huyu ni jirani yetu katika maeneo ya kazi hapa mbeya, na ni mtu tunayeshirikiana katika mambo mbali mbali.

 

 

 

SURA YA TANO

MATOKEO

 

Baada ya kukaa kwa muda mrefu bila kwenda shambani, kutokana sababu mbali mbali ikiwemo kutokuwa na nafasi, ufinyu wa bajeti, safari za hapa na pale nk. Lakini kwakweli tulikuwa na hamu ya kwenda kukagua maendeleo ya shamba. Hatimae siku moja mabwana wawili waliamua kwenda kuangalia maendeleo. Mr Ummar na bwana Ben Oiso walikwenda kuangalia maendeleo. Hii ilikuwa ni tarehe 31.03.2018 siku  ya jumamosi. Waliondoka mjini mnamo saa nne ya asubuhi.

 

Kwakweli mahindi yalikuwa yamefikia hatua ya kuliwa barabara. Na yalikuwa yameshaanza kunyauka kwa mbaaali. Ila kulikuwa na baadhi ya sehemu hazikua zinaridhisha hata kidogo. Lakini pia kuna sehemu zilikuwa zinaridhisha na kutia matumaini. Kama ambavyo uliona katika palizi kulikuwa na sehemu zilizo nzuri, wastani na sehemu nyingine zilikuwa ni mbaya zaidi. Na pia kama unakumbuka tulipanda mbegu za aina mbili ambazo ni SEEDCO na PANNAR. Mbegu ambayo haikufanya

vizuri ilikuwa ni PANNAR. Sehemu ya mbegu hii ilidhoofika kutokana na uhaba wa matunzo na si kwamba haifai.

 

Na mabwana hao waliporudi walileta takwimu kamili za picha kulingana na hali waliyoikuta huko shambani. Kama kawaida tutakuonesha picha halisi za siku hiyo walipo tembelea.

 

 

 

Huwezi kuamini - Hii ni sehemu ya shamba ambayo ilikuwa imedhoofika sana kutokana na majani kuyazidi mahindi. Hii ni sehemu kubwa iliyopandwa mbegu ya PANNAR                                (Picha na Omy Krish)

mahindi yakiwa yamedhoofika kutokana na kuzidiwa na majani

 

“Baba la baba” akiwa katika pirika pirika za kukagua mahindi. Hapo anaonekana akimenya hindi kwa ajili ya kwenda kulichoma.

“Baba la baba” akiwa sehemu ya shamba ambayo mahindi yake yapo vizuri mno.           Mkononi mwake amebeba mahindi aliyoyavuna kidogo kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.                             (Picha na Ben Oiso)

Mr Ben Oiso akiwa ameshika  rundo la mahindi mabichi. Kuhakikisha jambo linakwenda kama lilivotakiwa.(Picha na Omy Krish)

 

Vijana hawa waliporudi walikuja na mahindi ya kuchoma na tukanufaika nayo kama kawaida.

 

Tarehe 29.04.2018 siku ya jumapili tuliamua tena kwenda shambani kuangalia maendeleo. Na vile vile kujua kama mahindi yapo tayari kwa kuvunwa au bado.

 

Safari hii tulikwenda watu wawili ambao ni mimi (Bunduki) na bwana Ummar (Baba la baba). Na kama ulikuwa hufahamu, sisi ndio tulikuwa wenye shamba. Hivyo baadhi ya siku tulishindwa kuwapata ndugu zetu wahisani ambao walikuwa wanatusapoti katika safari zetu za shamba. Hii ni kutokana na majukumu yao binafsi.

 

Tuliondoka stendi kuu majira ya saa 4:52 asubuhi na kufika shambani mnamo majira ya saa 6:02 mchana. Baada ya kufika tulikwenda kwa mwenyeji wetu bwana Nick lakini hatukumkuta wala hatukukuta mtu yeyote pale nyumbani na kuamua kupandisha shambani.

 

Sasa hebu jionee mwenyewe shamba lilivokuwa likionekana kwa wakati huo.

Ukitazama kwa haraka unaweza ukadhani ni msitu wa AMAZON huko nchini Brazil,                       lakini HAPANA hili ni shamba, na huyu ni Baba la baba akikagua mahindi yaliosalia                    katika sehemu hiyo (Picha na Bunduki.com)

 

Picha unayoiona hapo juu ni sehemu ya shamba ambayo ilikuwa na majani mengi sana na ni miongoni mwa sehemu ambazo zilikosa palizi kwa muda muafaka. Kwahiyo hali ni kama hivo inavoonekana kwa kweli.

 

Baba la baba akitoa maelezo kwa ufupi kwa muandishi wetu juu ya kilimo. Na hapa ni akiwa sehemu ya shamba ambayo inaonekana kuwa na mazao mazuri. (Picha na Bunduki.com)

Mawazo ni sehemu ya maisha. Bunduki akiwa katikati ya shamba wakati wa ukaguzi. Anaonekana kuwaza jambo fulani tusilolifahamu. (Picha na Omy Krish)

 

Siku ile iliisha hivo. Kisha baada ya hapo tulijiandaa na kurudi nyumbani kwa ajili ya kujiandaa na siku ya kuvuna.

 

Mtihani ni kwamba katika mbegu zile mbili, SEEDCO ilikuwa tayari imeshakauka vilivyo wakati PANNAR ilikuwa bado kuna mahindi mabichi mabichi. Lakini kwa ushauri wa watu wa karibu, walisema kuwa ni bora tusubiri mahindi yakauke kabisa na tuvune kwa pamoja. Kwani kuvuna nusu nusu kungesababisha madhara kadhaa ikiwemo wizi wa mahindi yaliyobakia n.k.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

SURA YA SITA

MAVUNO

 

Mwishoni mwa mwezi wa tano na mwanzoni mwa mwezi wa sita tayari mahindi yetu yalikuwa yamesha kauka. Na tayari ulikuwa ni muda muafaka wa kuvuna, pia baadhi ya majirani zetu wa shambani walikuwa wameshaanza kuvuna. Lakini kwa upande wetu ilikuwa ni vigumu kuendelea na zoezi la kuvuna kwa sababu kipindi hiki kilikuwa ni kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani. Hivyo tuliona ni bora tuvute subira mpaka pale mwezi utakapokwisha.

 

Baada ya kwisha kwa mwezi wa Ramadhani tulijipanga haraka kwa ajili ya kuanza kuvuna. Siku ya tarehe 20 / 06 / 2018 sawa na siku ya jumatano zoezi lilianza rasmi. Tulizungumza na watu ambao wangetusaidia kuvuna na siku ilipofika walianza kazi rasmi.

Mr Ummar na kijana wake Ramadhani Chikumbii walielekea shambani mapema asubuhi ili kushirikiana na vijana ambao walipewa kazi ile ya kuvuna wakiongozwa na yule kijana anayeitwa Simon  kutoka kule kule Senjele.

 

TANBIHI

Kama unakumbuka katika mtiririko huu kuna Simon wawili. Wa kwanza ni Yule tulieanza naye kushirikiana tangu tunatafuta shamba. Huyu anaishi kijiji cha nyuma kidogo (NANYALA) kabla hujafika shambani.               Na Simon mwingine ni kijana wa kule kule kijijini.

 

Baadhi ya wavunaji wakielekea shambani kuanza kazi

Picha ya kunyapia ikiwaonesha vijana wakiwa katika harakati za uvunaji – kutoka kushoto ni Simon (wa NANYALA) na Mr Baba la baba (Picha na Ramadhan Chikumbii)

 

Baada ya kazi nzito -  wakiwa wamepumzika –                                                                                     kutoka kushoto ni Baba la baba akiwa na Simon

 

Watu wakiwa katika shughuli za upukuchuaji wa mahindi baada ya kuvuna.

 

 

Ilikuwa ni vigumu kumaliza shamba lote ndani ya siku moja kutokana na ukubwa pia kutokana na hali ya majani yaliyoko shambani. Hivyo zoezi la uvunaji lilichukua muda wa siku mbili (yaani jumatano na alhamisi). Siku ya mwisho iliwalazimu vijana hao kutafuta mashine ya kupukuchulia mahindi kabisa ili yalale yakiwa katika magunia. Kiukweli kazi hii ilikuwa kubwa sana hasa kwa siku hii ya pili. Lakini walikaza moyo na kufanikiwa kumaliza kazi kama ilivyokusudiwa ingawa walirudi nyumbani usiku.

 

Baada ya kuvuna mahindi yalisombwa na kuwekwa pale nje kwa bwana Nick, hii ni kwa ajili ya kusubiri ubebaji na kuyarudisha nyumbani.

 

Ilituwia vigumu kuyaleta mahindi kwa haraka nyumbani kwasababu mbali mbali hasa uhaba wa vyombo vya usafiri na nafasi kwa ujumla. Hii ilipelekea mahindi kukaa kwa muda mrefu shambani. Lakini tulizungumza na kiongozi wetu wa Galaxy bwana SALIM AL AMARY juu ya kutusaidia katika suala la usafirishaji. Lakini akasema kuwa tuvute subia kwani pindi itakapokuja gari ambayo inaleta mzigo tutaitumia hiyo na kuepusha/kupunguza gharama kubwa za usafirishaji.

 

Siku ya jumatatu tarehe 13/08/2018 ilikuwa ni siku ambayo tuliletewa mzigo mkubwa toka katika branch yetu ya Tanga. Mzigo huu ulikuwa na gari ya ofisi na dereva wetu bwana Mahamud Iyaka. Kwahiyo mnamo siku ya jumanne ya tarehe 14 tulielekea shamba na gari kwa ajili ya kuchukua mzigo wetu. Tuliondoka majira ya saa 12 jioni na kufika shamba majira ya saa moja usiku. Lakini pamoja na hayo ilitulazimu kwenda na mifuko mingine ya kuwekea mahindi kwa sababu pale yalikuwa yamekaa muda mrefu na mifuko ilikuwa tayari imeshachanika. Hivyo basi usiku ule ule ilitulazimu kuyafaulisha mahindi yale na kuyatia tena kwenye mifuko mingine na kushona. Hii ni kazi iliyotuchukua kama masaa mawili hivi. Hata ilipofika saa tatu ya usiku tulianza safari ya kurudi watu wakiwa wamechoka sana kuwa shunguli mbali mbali ikiwemo upakiaji.

Katika safari hii tulikuwa watu watatu ambao ni mimi, Ummar na dereva Iyaka. Baada ya hapo tulirudi nyumbani na kufika majira ya saa nne usiku.

 

Mpaka hapa zoezi zima la shamba lilikuwa limekwisha kwa. Na muda wa kukodisha mashamba ulikuwa umeshakaribia.

 

Hivyo basi: katika riwaya hii ya “TWENDE SENJELE” ambayo ilikuwa inazungumzia kilimo cha mahindi kwa msimu huu wa mwaka 2017/2018, itaishia hapa. Kuisha kwa kitabu hiki ndio maandalizi ya kitabu kingine ambacho kitaandaliwa katika msimu ujao wa mwaka 2018/2019.

 

Tunamshukuru Mwenyezimungu kwa kutuwezesha kufanikisha suala hili mpaka kufikia hapa tangu tumeanza siku ya kwanza mpaka leo.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

HITIMISHO

 

Shukrani za dhati ziwafikie:-

 

-         OMY KRISH                     :- Kiongozi wa msafara / Mpiga picha / Director

-         BEN OISO                          :- Mhariri / Afisa kilimo

-         SAIDI R. BUNDUKI          :- Mwandishi / Mchapishaji

-         NICKSON                            :- Mwenyeji wetu / Aliyetukodisha shamba

-         SIMON (Wa Nanyala)         :-Mtu aliyekuwa karibu nasi zaidi katika

                                                  shughuli  zote za shambani

-         ADAM NGOTTA (SMILE) :-Jirani aliyekuwa karibu nasi

-         SIMON (Wa Senjele)             :- Aliyekuwa kiongozi wa vijana wa kazi

                                                     kijijini (Senjele)

 

Bila kuwasahahu wana kijiji wote wa Kijiji cha Senjele wakiwemo wanakwaya ambao pia walichangia katika kuzorotesha zoezi zima la palizi.

Bila kumsahau Mtendaji wa kijiji kwa kutupa ushirikiano mzuri katika makabidhiano ya shamba na kadhalika.

 

Pia shukrani za dhati tunazitoa kwa Kampuni ya GALAXY COMPUTERS CO, LTD kwa kutoa ushirikiano mkubwa katika kufanikisha zoezi hili mpaka kufikia hapa ikiwemo msaada mkubwa wa vifaa vya uandaaji wa riwaya hii, usafiri, na ushauri pia katika kilimo.

 

Na mwisho shukrani ziwaendee wale wote ambao kwa namna moja au nyingie walishiriki katika kufanikisha suala hili ambao hapa sikuweza kuwataja bila kukusahau wewe msomaji wa Riwaya hii.

 

Asante.

 

COMMENTS

Follow - ili usipitwe

Kwa mawasiliano zaidi

Name

Afya,66,Blogging,18,Burudani,29,Dini,99,Maisha,38,Mashairi,52,Sitosahau,37,Teknolojia,7,Usichokijua,14,
ltr
item
mrbunduki: TWENDE SHAMBANI - (RIWAYA)
TWENDE SHAMBANI - (RIWAYA)
mrbunduki
https://sayyidbunduki.blogspot.com/2022/10/twende-shambani-riwaya.html
https://sayyidbunduki.blogspot.com/
https://sayyidbunduki.blogspot.com/
https://sayyidbunduki.blogspot.com/2022/10/twende-shambani-riwaya.html
true
3501413861140022348
UTF-8
Loaded All Posts Hakuna chapisho lolote View All Read more Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All Recommended posts LABEL ARCHIVE Search/Tafuta ALL POSTS Bahati mbaya, Ulichotafuta hakipo Rudi nyumbani/Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content